27 Desemba 2025 - 15:13
Mashia wa Pakistan waonyeshe taswira halisi ya Ushia kupitia maadili, tabia, na matendo yao ya kila siku

Ayatollah Sistani Mkuu, akiombea kwa ajili ya waumini wote wa Pakistan, hasa waumini wa Gilgit-Baltistan, alisisitiza kuwa Waishe Shia wa Pakistan wanapaswa kuishi kwa umoja na mshikamano, na kupitia maadili, tabia, na matendo yao ya kila siku, wape taswira halisi ya Uislamu halisi wa Mtume Muhammad (saww) unaofuatwa na waislamu wa Madhehebu ya Shia.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA- Sheikh Muhammad Hasan Jafari, Imam wa Ijumaa wa Skardu nchini Pakistan, alikutana na Ayatollah Sistani Mkuu, Kiongozi na Marjii wa juu wa Mashia, katika Mji wa Najaf Ashraf na kufanya naye mazungumzo kuhusu masuala ya kielimu na kidini.

Katika mwanzo wa mkutano huu, Ayatollah Sistani (aliomba) dua kwa ajili ya Waumini wote wa Pakistan, hasa Waumini wa Gilgit-Baltistan, na kusisitiza kuwa Mashia wa Pakistan wanapaswa kuishi kwa umoja na mshikamano, na kupitia maadili, tabia, na matendo yao ya kila siku, waonyeshe taswira halisi ya Uislamu Halisi wa Mtume Muhammad (sawww) unaofuatwa na Madhehebu ya Shia Ithna Ashari.

Aidha, Ayatollah Sistani alikadiria sana huduma za kidini, kielimu na kijamii za Sheikh Muhammad Hasan Jafari.

Katika mkutano huo, mtoto wa Sheikh Muhammad Hasan Jafari pia alihudhuria.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha